Msemaji wa rais, Harry Roque , amesema serikali haikubaliani na mahitimisho yanayofanywa na baadhi ya wataalamu wa Ufilipino kuwa China inaongeza hali ya wasiwasi katika bahari hiyo katika wakati nchi zinajishughulisha zaidi na kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19.
Tangu Februari, China imekuwa ikipeleka meli, vyombo vya utafiti na meli za ulinzi wa pwani katika eneo hilo la kiuchumi la Ufilipino, Vietnam na Malaysia, katika hatua inayozidisha azma yake ya kuyachukua maeneo katika bahari hiyo, wataalamu wamesema.
Jaji wa zamani wa mahakama kuu ya Ufipino, Antonio Carpio, aliandika katika mtandao wa kijamii jana kwamba inasikitisha kwamba China inafanya hivi katika wakati huu wa janga la corona.

0 Comments
+255717114144