Museveni aliwataka wamiliki wa nyumba wawe wavumilivu kwa kuwa janga la corona linamuathiri kila mmoja.
Alisema kitendo cha wamiliki wa nyumba kuwafukuza wapangaji wanaoshindwa kulipa kodi hakikubaliki.
Wiki iliyopita Rais Museveni alitangaza amri ya kutotoka nje na kusalia nyumbani kwa siku 14 kuanzia 1.000 usiku hadi 12.00 asubuhi.
Pia, Rais Museveni alipiga marufuku watu kuendesha magari yao isipokuwa ya kusafirisha mizigo na kutokufunguliwa kwa maduka na kuruhusu biashara ya vyakula pekee.

0 Comments
+255717114144